Friday, 10 June 2016

DE GEA AKATAA KUHUSIKA KWENYE KESI YA NGONO .




Kipa wa Man United David De Gea.


Mwangi K.Githinji.

David de Gea amepuzilia mbali madai kwamba alihusika katika kesi ya ngono huku akisisitiza kuwa atasalia na timu ya Uhispania kwenye michuano ya yuro.
Tuhuma hizo ziliibuliwa hii leo zikiwa zimesalia siku tatu tu kabla ya kuanza kampeni ya taifa la Uhispania kwa mechi dhidi ya Czech Republic.
Katika ripoti ya polisi shahidi mmoja aliye chini ya ulinzi mkali anayedai kwamba alilazimishwa kushiriki tendo la ndoa bila hiari yake kwenye hoteli mmoja iliyoko mjini Madrid iliyokodishwa na Allende Fernandez hali maarufu Torbe aliye korokoroni na ambaye kwa kuhusika na filamu za ngono.
Japo De Gea anaelezewa kutokuwepo katika eneo la tukio shahidii huyo amedhibitisha kwamba kipa huyo wa Manchester United alihusika kuandaa  mkutano huo akishirikiana na Torbe.
Aidha mlinda lango huyo ameeleza kuduwazwa na taarifa hizo alipofanya kikao na wanahabari.


No comments: