Monday, 6 June 2016

MAANDAMANO YA IEBC TAYARI YA SHUHUDIWA BAADA YA KUONYWA NA INSPEKTA WA POLISI..

vijana wanawasha matairi moto
Na David Muli.

Shule kadhaa na biashara zimefungwa mtaa  wa Kibera hapa Nairobi huku maandamano dhidi ya tume ya IEBC yakitayarjiwa kufanyika  jijini.

Tayari vijana wamewasha matairi katika barabara kadhaa za Nairobi ikiwemo ya Jogoo na Uhuru.

Kwingineko maandamano yameanza kaunti ya Migoro barabara ya Sirare kuelekea Kisii ikifungwa.

Polisi wameonya kuwa watawakabili vikali watakaodhubutu kuandamana hapa Nairobi. Inspekta mkuu wa polisi Joseph Boinet amewataka wanaCORD kuheshimu agizo la mahakama na kusimamisha maandamano hayo.

No comments: