![]() |
| Mchezaji Messi. |
Na Mwangi K .Githnji.
Nyota wa timu ya Argentina na klabu cha Barcelona Lionel
Messi ametangaza kuwa amestaafu soka la kimataifa baada ya timu yake ya
Argentina kulazwa na Chile kwenye fainali ya Copa America .
Messi mwenye umri wa miaka 29 ameeleza kuwa
alilazimika kuacha kulichezea taifa lake kwani ameshindwa kulisaidia kutwaa
taji lolote.
Alikiri kuwa ilimuuma sana hasa ikizingatiwa kuwa
ameambulia patupu tangia alipoanza kuiwakirisha Argentina mnamo mwaka wa 2005.
Ilikuwa
ni mara ya nne kwa mchezaji huyo aliyeichezea Argentina mechi 112 kupoteza
katika awamu ya fainali.

No comments:
Post a Comment