Wednesday, 8 June 2016

MOURINHO AMSAJILI MLINZI ERIC 'BAILLY' .



Sajili mpya wa United Eric Bertrand Bailly.





Mwangi K. Githinji.

Klabu cha Manchester United kimekamilisha usajili wa mlinzi Eric Bertrand Bailly kutoka Villarreal ya Uhispania ,japo bado hajapata stakabadhi zinazomruhusu kuichezea United.
Bailly amejiunga na United kwa mkataba wa miaka minne baada ya kufanyiwa vipimo vya afya hii leo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, aliichezea Villarreal mara  47 msimu jana tangia alipohamia klabu hicho mnamo mwaka wa 2015.

Kwa upande mwingine ameweza pia kuichezea Ivory Coast katika mechi 15 na alikuwa kwenye kikosi kilichotwaa kombe la mabara ya Afika mwaka wa 2015.

No comments: