Mwangi K. Githinji.
Kiungo wa AS Roma Radja Nainggolan amefichua kuwa
mastaa wa Chelsea Eden Hazard na Thibaut Courtois wanamshawishi ajiunge na
miamba hao wa uingereza msimu ujao.
Mbelgiji
huyo anayechezea taifa la Ubelgiji pamoja na mastaa hao wawili ameelezewa kuwindwa na mkufunzi mpya wa Chelsea Antonio Conte huku Naiggolan akifichua kuwa tayari amekutana na Conte.
Naiggolan
amekiri kuwa Conte anamuangazia japo ameeleza kwamba kwa sasa anawazia tu
kulichezea taifa lake, katika michezo ya yuro ya mwaka huu.


No comments:
Post a Comment