Mwangi K. Githinji.
Staa wa Chelsea Pedro Rodriguez
amekiri kuwa angetaka kurejea tena katika klabu cha Barcelona baada ya kufanya mazungumzo na Rais
wao kuhusu uwezekano wake wa kurudi Camp
Nou.
Pedro amefichua alivyotamaushwa na
kughura kwake kutoka Barca japo amefichua kwamba hakuwa na budi kwa kuwa
alikuwa anataka kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza.
Akiwa na wanacatalunha hao winga
huyo mwenye umri wa miaka 29 alifunga mabao 48 na aliibuliwa
kutoka kwa timu yao ya chipukizi.
Iwapo ataondoka itakuwa ni pigo kwa
mkufunzi mpya Antonio Conte ambaye anatarakiwa kutua Stamford Bridge baada ya michezo ya
yuro ili kukinoa klabu hicho cha nchini uingereza.

No comments:
Post a Comment