Ajenti wa nyota Paul Pogba amekiri kuwa
amefanya mazungumzo na klabu cha Liverpool.
Katika mechi 178
alizoichezea Juventus Pogba mwenye umri wa miaka 23 amewafungia mabao 34 baada
yake kughuria Serie A akutoka Manchester united mnamo mwaka wa 2012.
Mino Raiola amesema kuwa amefanya pia mazungumzo na vilabu kadhaa vya uingereza na kile cha Real Madrid ambacho kinasemekana kuwa karibu
kutwaa sahihi yake.
Mchezaji huyo ana
dhamana ya yuro milioni 123 japo huenda ikawa vigumu kwa Liverpool kumnunua
kutokana na ushindani mkali kutoka kwa united na Madrid.

No comments:
Post a Comment