Thursday, 30 June 2016

SIO SIRI TENA,NAHAMIA MAN UNITED-IBRAHIMOVIC.

Mchezaji Zlatan Ibrahimovic.
Mwangi K. Githinji.

Nyota wa Sweden Zlatan Ibrahimovic amedhibitisha kuwa atajiunga na klabu cha Manchester United kwenye majira haya ya joto.
Mshambuliaji huyo alichapisha ujumbe kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii ambapo alifichua habari hizo  masaa machache tu baada ya united kuratibu mechi ya matayarisho ya msimu ujao nchini Sweden.
Lakini bado staa huyo mwenye umri wa miaka 34 hajasaini mkataba wowote na miamba hao wa uingereza ambapo anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya wiki ijayo.


Zlatan amewahi kufanya kazi tena na Mourinho walipokuwa klabuni cha Inter Milan na ataungana na sajili mpya wa mashetani hao wekundu Eric Bailly.

No comments: