![]() |
| Mlinda lango wa Arsenal Cech. |
Na Mwangi K.Githinji.
Mchezaji wa Arsenal Peter Czech
amekiri kutamaushwa na msimu wake wa kwanza na miamba hao baada ya klabu hicho
kuambulia bila taji lolote msimu jana.
Nahodha huyo alihamia Arsenal kutoka Chelsea kwa
kima cha yuro milioni 11 kutokana na ushindani mkali kutoka kwa kipa mwenzake
Thibaut Courtois.
Na japo wanabunduki hao walianza vizuri msimu kwa
kushinda taji la community Shield baadaye walishindwa kufana kwenye ligi kuu ya
uingereza.
Amesema kuwa mwanzoni walidhani kuwa walikuwa na
kikosi bora ambacho waliamini kingepigania taji la ligi lakini hatimaye
Leicester wakawapiku na hivyo kulishinda.

No comments:
Post a Comment