![]() |
| Mchezaji Luis Nani yuko nchini ufaransa na timu yake ya ureno. |
Na Mwangi K. Githinji.
Klabu cha Valencia kimedhibitisha kuwa kimemsajili aliyekuwa
winga wa Manchester United Luis Nani kutoka Fenerbahce.
Valencia wamemtwaa kwa kima cha yuro milioni 8.5 ambapo
amesaini mkataba wa miaka mitatu.
Akiwa Fenerbahce alicheza mechi 46 huku akiwafungia
mabao 12 msimu mzima.
Kwa sasa Nani yuko nchini Ufaransa ambapo analiwakilisha
taifa lake la ureno kwenye mashindano yanayoendelea ya yuro wakiwa wameratibiwa
kuchuana na Wales katika awamu ya nusu fainali.
Licha ya sahihi yake kuwaniwa na vilabu kadhaa vya
uingereza ikiwamo Stoke City na Everton amefanya uamuzi wa kuhamia Valencia
ambao wanashiriki ligi ya uhispania.

No comments:
Post a Comment