Tuesday, 5 July 2016

WAZIRI MKUU WA TANZANIA APIGA MARUFUKU SHISHA.


Shisha ambayo pia hujulikana kama hookah hutumiwa sana Uarabuni na bara Asia.


Ben Kirui

Serikali ya Tanzania imepiga marufuku uvutaji wa shisha nchini humo na kulitaka jeshi la polisi kufanya kila juhudi kutokomeza uraibu huo.

Waziri mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa agizo hilo na kusema uvutaji shisha umekuwa ukichangia katika kudorora kwa maadili miongoni mwa vijana, na kuwapunguzia uwezo wa kiakili na kimwili wa kufanya kazi.

Majaliwa amesema watakaokaidi agizo hilo pamoja na wauzaji wa vilevi hivyo, wataadhibiwa vikali.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alikuwa ametangaza kuwa ni marufuku watu kuvuta shisha hadharani iwe ni katika baa, klabu au eneo lolote la starehe.
 

No comments: