Tuesday, 5 July 2016

FBI KUCHUNGUZA MAUWAJI YA WAKILI WILLIE KIMANI

Kutoka kulia: Mwendazake wakili Willie Kimani, mteja wake Josphat Mwendwa na dereva wa teksi Joseph Muiruri

 Ben Kirui

Maafisa wa upelelezi kutoka marekani FBI watasaidia katika uchunguzi wa mauwaji ya wakili Willie Kimani, mteja wake Josphat Mwendwa na dereva wa teksi Joseph Muiruri.

Mkurugenzi wa CID Ndegwa Muhoro amehakikishia mahakama kwamba uchunguzi wa mauwaji hayo utakamilika kwa siku 14 zijazo.

Hata hivyo wakili wa chama cha mawakili nchini LSK Charles Kanjama amesema ripoti hiyo ya Muhoro haina msingi huku akitaka wapewe nafasi ya kumuuliza maswali.

Wakati huo huo afisa wa polisi Leonard Mwangi alifikishwa mahakamani na kuwekwa rumande kwa muda wa siku 13 ili kuwapa polisi kukamilisha uchunguzi.

No comments: