Monday, 4 July 2016

MATUIDI AONDOKA KAMBI YA UFARANSA KUJIUNGA NA MIAMBA WA UINGEREZA.


Mchezaji Blaise Matuidi.
Na Mwangi K. Githinji.
Kiungo wa Paris Saint-Germain Blaise Matuidi aliondoka kutoka kwa kambi ya timu yake ya taifa ya Ufaransa  hapo jana na kusafiri moja kwa moja hadi uingereza ili kuutatua mustakabali wake.
Habari hii imewaacha wengi wakijikuna vichwa kuhusu klabu atakachokighuria kwa kuwa hakuweka wazi mipango yake.
Haijulikani kama atajiunga na Manchester United,Manchester City ,Arsenal ama pengine hata klabu kingine kinachocheza kwenye ligi kuu ya EPL.
Matuidi mwenye umri wa miaka 29 anawakilishwa na ajenti Mino Raiola ambaye pia anamuwakilisha staa Zlatan Ibrahimovic ambaye tayari amejiunga na Manchester united.

No comments: