![]() |
| Vijana wa Kenya chini ya umri wa miaka 17. |
Na Mwangi K. Githinji.
Mchezaji
wa Malawi alifunga magoli matatu na hivyo kuwasaidia mababe
hao kuicharaza timu ya Kenya chini ya umri wa miaka 17 katika mechi ya
michuano ya COSAFAiliyochezwa hapo jana.
Licha ya dimba hilo kumalizika bao 1-0 katika kipindi cha
kwanza vijana wa Kenya walishindwa kubadilisha matokeo hayo ijapokuwa walifanya
mabadiliko kadhaa huku mchezo huo ukiishia mabao 5-0.
Kenya walifungwa mabao kumi kwenye mechi tatu
walizocheza ndani ya dimba hilo ambapo walianza kwa kupoteza 4-0 dhidi ya Zambia na kisha baadaye mabao
2-1 walipokabiliana na Madagascar.

No comments:
Post a Comment