Monday, 18 July 2016

KAHABA ATOROKA NA BASTOLA YA MLINZI WA GAVANA.



 Ben Kirui

Polisi mjini Nakuru wanamsaka kahaba mmoja anayedaiwa kuiba bastola ya mlinzi wa gavana wa Turkana Josphat Nanok bastola iliyopotea mwishoni mwa juma mjini Nakuru.

Akithibitisha kisa hicho Ocpd wa Nakuru Joshua Nkanatha amesema kuwa mlinzi huyo Benjamin Lorum ambaye ni afisa wa polisi katika kituo cha polisi cha Lodwar aliipoteza bastola hiyo iliyokuwa na risasi kumi na tano pamoja na shillingi elfu 14 baada ya kuwa na kahaba huyo katika danguro moja mjini Nakuru.

Nkanatha amesema mlinzi huyo alikuwa ameandamana na gavana Nanok hadi Nairobi kwa shughuli rasmi za kikazi kabla ya kuomba siku ya mapumziko ijumaa na kuelekea Nakuru.

Lorum alipatikana bila nguo wala viatu na akiwa amepoteza fahamu huku kahaba akiwa ametoweka.

No comments: