Monday, 18 July 2016

POLISI WANNE WASHTAKIWA KWA MAUAJI YA WAKILI.


Mawakili na wananchi  wakifanya maandamano mjini Nairobi
Na Ben Kirui

Polisi wanne wa utawala wameshtakiwa kwa mauwaji ya wakili Willie Kimani, mteja wake Josphat Mwenda na dereva wa teksi Joseph Muiruri.

Maafisa hao wa Ap Fredrick Leliman, Leonard Mwangi, Silvia wanjiku na Stephen Cheburet hata hivyo wamekana mashtaka mbele ya jaji Jessie Lessit katika mahakama za milimani hapa jijini Nairobi.

Jaji Lessit ameamuru wanne hao wazuiliwe rumande kwa siku 30 wakisubiri mahakama kuamua ombi lao la kutaka kuachiliwa kwa dhamana.


Kikosi cha majasusi kutoka humu nchini na marekani Kinaamini kuwa wanne hawa walihusika katika mauaji ya Kimani na wenzake katika eneo moja karibu na kambi ya polisi wa utawala ya Syokimau baada ya kukamatwa na kuzuiliwa katika kambi hiyo mwezi uliopita.

No comments: