![]() |
| Mbrazili Willian. |
Na Mwangi K. Githinji
Kiungo wa Brazil Willian amesaini
mkataba mpya wa miaka minne utakaombakiza ugani Stamford Bridge hadi mwaka
wa 2020.
Tayari the Blues wamemsajili mchezaji Michy Batshuayi na nyongeza hiyo ya mkataba itakuwa ni afueni kwa mkufunzi mpya Antonio Conte ambaye amechukua hatamu klabuni Chelsea hivi majuzi.
Willian alikuwa mchezaji bora wa
klabu hicho msimu jana licha yao kusajili msururu wa matokeo mabaya ligini kuu
uingereza.
Ilikuwa inakisiwa kuwa nyota huyo angehama Chelsea huku tetesi zikimhusisha na kughuria Manchester United.
Ameeleza furaha yake baada ya kusaini kandarasi na timu hiyo aliyojiunga nayo miaka mitatu iliyopita akisema kuwa anapania kuendelea kuisaidia kushinda mataji mengi zaidi.

No comments:
Post a Comment