![]() |
| Joseph Muthaiga chifu wa eneo la Makuyu. |
Robert Mwangi
Polisi katika kaunti ya Vihiga
wameanzisha msako wa mwanamume mmoja ambaye anadaiwa kumuua mwanawe wa kiume
mwenye umri wa miaka minane kwa tuhuma za kuiba shillingi 1000
Inadaiwa kwamba Mwanamume huyo
mwenye umri wa miaka 45 kutoka kijiji cha Mwiitoko alimchapa mwanawe hadi akafa
baada ya pesa alizopata kutokana na kuuza kuku kutoweka.
Kule Maragwa katika kaunti ya
Muranga mwanamume mmoja amemuua mkewe pamoja na wanawe wawili kwa kile
kinachokisiwa kuwa mzozo wa kifamilia.
Mwanamume huyo mwenye umri wa
miaka 30 alitumiwa panga kutekeleza unyama huo na kisha kujitia kitanzi. Chifu
wa eneo hilo amesema kuwa tukio hilo limeripotiwa kwa polisi ili uchunguzi
uanzishwe.

No comments:
Post a Comment