Tuesday, 15 November 2016

BARAZA LA WIPER LAPUUZILIA KUWEPO KWA UFA KATI YA KALONZO NA MUTHAMA.

Kalonzo Musyoka na Johnson Muthama
Robert Mwangi.

Baraza kuu la chama WIPER limedinda kueleza kuwa iwapo dhana inayoendelea kuwa kiongozi wa chama hicho Kolonzo Musyoka na seneta wa Machakos Johnson Muthama  walitofautiana siku ya Ijumaa katika ziara ya Kolonzo huko ukambani.

Duru ziliarifu kuwa Kolonzo na Muthama walikosana baada ya Muthama  kusema  kuwa chama cha muungana Party kinachoongozwa na gavana Kibutha Kibwana hakifai kuwa na wagombeaji katika eneo la ukambani madai ambayo chama hicho kimekanusha.

Aidha Muthama anadaiwa kuwa ana mpango wa kuzima ndoto ya Kalonzo ya kuwa mwaniaji wa urais kupitia CORD  na badala yake kumuunga mkono Raila Odinga wa ODM.

Muthama hakuhudhuria kikao hicho cha Wiper na  badala yake alikuwa katika mkutano mwingine wa CORD uliokuwa ukijadili masuala ya IEBC.


No comments: