Tuesday, 15 November 2016

DIER KULIPIZA KISASI DHIDI YA HERRERA WA MAN U

Eric Dier akimsogelea Ander Herrera baada ya tukio hilo (Picha: Getty)

KAPEDO JNR
Kiungo wa timu ya taifa ya Uingereza almaarufu “the three lions” muite Eric Dier, amesema kuwa atalipiza kisasi dhidi ya mchezaji Ander Herrera, dakika tano kabla ya mechi hio kukamilika, mechi ambayo Uingereza ilitoka sare ya kufungana magoli mawili kwa mawili dhidi ya Uhispania hapo jana usiku.

Dier, ambaye ana miaka ishirini na mbili alisema, “nafikiri ni wazi kwamba alinipiga kumbo, sababu nahisi maumivu kwa shavu langu, kwa hivyo najua alivyofanya, na sikupendezwa na kitendo hicho”

Aidha Dier aliongezea kuwa, “Sina shida na watu kupigana mateke wakati mwingine lakini hicho ni kitendo cha unyama na hakistahili”

Manchester United itaialika Tottenham Hotspurs ugani Old Trafford kwenye mechi ya kuwania kombe la EPL tarehe 11 Disemba 2016


No comments: