![]() |
KAPEDO JNR
Mshambulizi wa klabu ya Kariobangi
Sharks Ibrahim Kitawi amefichua kuwa timu hio inapanga kuhifadhi alama zote za
mechi zinazosalia kwa kuepuka makosa modogo ili kuongeza matumaini yao ya
kupanda kwenye ligi kuu humu nchini KPL
Sharks wameandikisha matokeo ya
kufana tangu walipotoka sare ya kutofungana dhidi ya Nakumatt tarehe 24 Oktoba 2016,
huku wakijitahidi kuandikisha matokea mazuri kwa mechi zilizosalia jambo ambalo
limewapelekea kupanda hadi nafasi ya pili kwenye jedwali la ligi kuu nchini KPL.
Kitawi ameifungia Sharks mabao
sita kwenye michuano minne ya hivi karibuni huku akisalia mfungaji bora wa
klabu hio msimu huu akiwa na mabao kumi na mbili.
Oserian itaialika Sharks kwenye
mechi ya kuwania kombe la Supa League ambayo imeratibiwa kuchezwa jumaapili hii
tarehe 14 Novemba 2016

No comments:
Post a Comment