Thursday, 10 November 2016

LAIKIPIA:WITO WATOLEWA KWA SERIKALI KULETA HUDUMA ZA BODI YA NAFAKA KARIBU NAO.

Kundi la wakulima katika kaunti ya Laikipia.
Na Mwangi K.Githinji

Wakulima kutoka maeneo ya Ng’arua na Kinamba kwenye kaunti ya Laikipia wametoa wito kwa serikali ya taifa kuleta huduma za bodi ya mazao na nafaka karibu nao.

Wakulima hao wamelalamikia kupunjwa na wanunuzi ambao wamedai hununua mazao yao kwa bei duni jambo ambalo wanahisi kuwa linaweza likarekebishwa ikiwa serikali italeta bodi hiyo katika eneo hilo.


Aidha wamesema kuwa ikiwa serikali itatilia maanani suala hilo basi itakuwa ni afueni kubwa kwao kwa sababu wanahisi kana kwamba bei za chini kwa mavuno yao zinakandamiza na kuhujumu juhudi zao kama wakulima.

No comments: