![]() |
| Vifusi vya jengo lililoporomoka |
Robert Mwangi
Jumba
la orofa tisa ambalo ujenzi wake ulikuwa ungali unaendelea liliporomoka huko Kisii na kuleta
maafa ya watu sita akiwemo mtoto wa miaka kumi na mitano.
Wananchi waliofika eneo la mkasa walitatiza pakubwa shughuli ya ukoaji iliyokuwa ikiendeshwa na shirika la msalaba
mwekundu chini ya ulinzi wa polisi.
Zaidi ya watu arubaini wameokolewa na mashirika ya
uokoaji huku mashirika hayo yakiendelea na shughuli ya ukoaji wakisema kuwa
wana matumaini kuwa wataweza kupata watu zaidi wakiwa uhai.
Ujenzi wa
jumba hilo umekosolewa na wengi hasa ikizingatiwa kuwa halmashauri ya ujenzi wa
manyumba ilikuwa imeharamishwa ujenzi wa jumba hilo kama alivyokiri fundi mmoja aliyekuwa akishiriki
ujenzi wa jumba hilo.

No comments:
Post a Comment