Monday, 14 November 2016

LAMPARD KUGURA NEW YORK CITY FC

30 Ocktoba 2016; Toronto, Kiungo wa New York FC Frank Lampard (8) awania mpira dhidi ya kiungo wa klabu ya Toronto FC Will Johnson (7), kwenye kipindi cha pili uwanjani BMO, mechi ambayo Toronto ilishinda kwa magoli 2- 0
Picha: Dan Hamilton-USA TODAY Sports

Kiungo wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza na miamba wa ligi kuu ya Uingereza Chelsea, muite Frank Lampard ataigura klabu hiyo mwezi ujao, Disemba

Mnamo jumaatatu kupitia kwa mtandao wao (www.nycfc.com), klabu hiyo ilitangaza kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 ataihama klabu hiyo baada ya mkataba wake kukamilika mwisho wa mwaka huu, 2016

Lampard alisajiliwa na klabu ya New York mwaka wa 2014, huku akitia wavuni magoli 15 kwenye mechi 31 alizochezea klabu hiyo.

Lampard alinukuliwa akiwashukuru mashabaiki wa klabu hiyo kwa uungwaji mkono na ukarimu wao waliodhihirisha kwa klabu hiyo kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita

No comments: