Tuesday, 22 December 2015

MWANAMKE AFUNGWA MIAKA 5 KWA KUSHIKA MIMBA!!!!

Na KakaMusa,



A Pregnant Woman
Mwanamke wa Uganda ambaye anafanya kazi nchini Kuwait amehukumiwa kifungo cha  miaka 5 pamoja na mwanawe  kwa kosa la kushika mimba nje ya ndoa.

Nambi Fatumah alifikishwa mahakamani miezi kadhaa iliyopita na kushtakiwa kwa kosa hilo.

Kulingana na mwenyekiti wa chama cha Waganda wanaoishi nchi za bara Asia, Ali Nusbuga, Fatuma angeokolewa ikiwa serikali ya Uganda na mashirika ya haki kwa binadamu yangeingilia kati.

Nchini Kuwait, mwanamke hafai kupata mtoto kabla ya kuolewa ama nje ya ndoa na yeyote anayekiuka sharia hii, yeye hufungwa jela bila kujali dini, rangi wala alikotoka.

Nusbuga anaiomba serikali ya Uganda kuingilia suala hili na kutumia diplomasia ili kumrejesha nyumbani Fatumah au hata kumpunguzia kifungo hicho. #Asante.

No comments: