Tuesday, 22 December 2015

RAILA ASIMAMA TISTI NA MSIMAMO WAKE, KUHUSU HAWALA YA EUROBOND

NA JULIUS KARIITHI

Kinara wa Cord Raila Odinga na Rais wa jamhuri ya

Kenya Uhuru Kenyatta

Kinara wa Cord angali ameshikilia msimamo wake kuwa shilingi billioni  140 za hawala ya EuroBond hazijulikani zilipo.
Odinga alisema haya wakati wa mahojiano katika kituo kimoja cha talevisheni hapa nchini, huku akidai kuwa serikali imekuwa ikicheza kayaya za chini kwa chini, kuhusu vile ambavyo imechukulia swala la EuroBond ,waama hesabu zenyewe haziafikiani, hivyo kuwaacha wakenya na maswali mengi kuliko majibu.

Kiongozi huyu amekuwa mpiga filimbi kwenye swala hilo kwa miezi kadhaa iliyopita ,na kusema kuwa taarifa za benki zilizotolewa na serikali kutoka benki ya JP Morgan ,sio kamilifu na kuwa zimeacha maswali mengi vile vile  mianya mingi.



No comments: