Friday, 8 April 2016

MAAFISA WA KENYA NA UGANDA KUJADILI MZOZO KUHUSU MIGINGO

Kisiwa cha migingo
Ben Kirui

Huenda mzozo baina ya Kenya na Uganda ukatatuliwa wakati ambapo maafisa wa nchi zote mbili watakutana kwa majadiliano wiki ijayo.
Kamishna wa eneo la Nyanza Wilson Njenga amesema vikundi hivyo viwili vya maafisa wa usalama vitakutana kampala Uganda jumatano ijayo.
Njenga amekariri kuwa mzozo huo ni suala kati ya mataifa mawili na mapatano kati ya serikali zote mbili yatasaidia sana kufanikisha suluhu kuhusu umiliki wa kisiwa hicho.
Kisiwa cha Migingo kimekuwa kikizozaniwa na Kenya na Uganda kwa miaka kadhaa.


1 comment:

Anonymous said...

Migingo belongs to kenya. Period!