Tuesday, 5 April 2016

MWANAMME AMUUA MKEWE KISHA KUMTEKETEZA MWANAWE

Polisi wanachunguza kisa cha mwanamme kumuua mkewe
Ben Kirui

Polisi eneo la Koibatek kaunti ya Eldama Ravin wanachunguza kisa ambapo mwanaume mmoja amemuua mkewe na kisha kumteketeza mwanawe.
Kulingana na polisi na wenyeji wa kijiji cha Moringwo, mwanamme huyo Moses Keitany alimgonga mkewe kwa kichwa mara kadhaa akitumia chuma akimuua papo hapo.
Walioshuhudia kisa hicho wamesema kuwa mwanamme huyo alimchukua mwanawe wa miaka saba baada ya kutekeleza unyama huo na kujifungia kwa nyumba kabla ya kuiteketeza.

Hata hivyo, waliokolewa na majirani na kukimbizwa katika hospitali kuu ya Rift Valley.

No comments: