![]() |
Waziri wa elimu Dkt .Fred Matiang'i , aliyatangaza matokeo ya mtihaniwa KCPEleo tarehe 30 Desemba 2015 |
Shule za kibinafsi zimefanya vyema zaidi
katika mtihani wa kitaifa wa kcpe kuliko shule za umaa ,wakati matokea hayo
yametangazwa rasmi hii leo.
Waziri wa elimu, Dkt Fred Matiang’i, dakika chache zilizo pita
ameonyesha kuwa matokea ya jumla, yameshuka kwa alama saba ikilinganishwa na ya mwaka uliopita, japo hajazungumzia kwa kina
matokeo hayo ya mtihani huo,huku alimkabidhi wakurugenzi wa elimu katika kila
kaunti matokeo hayo.
Aidha waziri huyo ameipa changamoto idara husika ya mtihani wa
kitaifa Knec, kuchukua hatua kali kwa wanaopatikakani wakijihusisha na wizi wa
mtihani, huku akisema kwambi hakuna njia nyingine ya kujinasua.
Kwa sasa wazazi na wanafunzi waweza kupata matokeo hayo kwa
kutuma nambari zao za usajiri wa mtihani ,kupitia nambari ifuatayo 22252.

No comments:
Post a Comment