![]() |
Afisa mkuu mtendaji wa tume ya mitihani, knec Joseph Kivilu awaliakihutubia wanahabari |
Tusisalia kwenye
maswala ya elimu Afisa mkuu mtendaji wa tume ya mitihani ya kitaifa, Joseph
Kivilu, amesema kuwa takriban watu 157 wamefunguliwa mashtaka kwa kujihusisha
na wizi wa mitihani.
Akizungumza wakati wa matokeo ya mtihani wa kitaifa wa KCPE hii
leo, Kivilu amesema kuwa aliofungwa and kuhukumiwa kwa wizi huo wa mtihani ,ni
pamoja na wakuu wa shule, manaibu wao, wanafunzi wa vyuo, wazazi, maafisa wa
polisi pamoja watahiniwa wenyewe.
Kivilu hivi majuzi alisema kuwa hakutakuwa na kuorodheshwa kwa
shule na mtindo wa kuyatangaza matokea utakuwa tu kama wa mwaka uliopita.
Mtihani huo wa kitaifa wa KCPE ulijumuisha takriban watahiniwa
937,467 kote nchini.

No comments:
Post a Comment