Wednesday, 27 January 2016

JSC YATEUA JOPO KUMCHUNGUZA JAJI TUNOI


Jaji mkuu Willy Mutunga

 Na Ben Kirui

Tume ya Huduma za Mahakama JSC imeteua jopo la maafisa 6 kuchunguza tuhuma za ulaji rushwa ya milioni 200 zinazomkabili jaji wa mahakama ya juu Philip Tunoi.
Rais wa JSC Jaji mkuu Dkt Willy Mutunga ametangaza hayo baada ya kikao maalum cha dharura kilichoitishwa kufuatia hatua ya Bw Geoffrey Kiplagat kupasua mbarika kuwa yeye ndiye aliyefanikisha hongo ya shiilingi millioni 200 kwa jaji Tunoi ili awashawishi wenzake kupendelea upande mmoja wakati wa uamuzi wa kesi ya kupinga uchaguzi wa gavana wa Nairobi Dkt Evans Kidero.
Jopo hilo linajumuisha mkuu wa sheria Prof Githu Muigai, Mkuu wa tume ya utumishi wa umma Prof Margaret Kobia, jaji Aggrey Muchelule, Bi Emily Ominde, Bi Winnie Guchu na Bw Kipkorir Bett.
Sita hao wanapaswa kukamilisha uchunguzi huo na kutoa taarifa kwa tume ya JSC inayosimamia maswala ya haki na mahakama nchini katika kipindi cha siku saba sijazo.
Aidha Jaji Phillip Tunoi na Gavana Evans Kidero wamejitokeza wazi wazi na kukanusha tuhuma hizo.


No comments: