Wednesday, 20 January 2016

MAAFISA SABA WA POLISI WATIMULIWA


Mwenyekiti wa NPSC na wanakamati wa Tume ya NPSC
 BEN KIRUI

Maafisa saba wa polisi wameachishwa kazi na Tume ya Kitaifa ya Huduma za Polisi NPSC baada ya kufichuliwa kwamba walitumia vyeti ghushi wakati wa usajili wa polisi.
Utovu wa nidhamu wa afisa msimamizi wa polisi wa kitengo cha utawala Nelson Omwega ilibainika leo wakati Tume ya kitaifa ya huduma za polisi ilikuwa ikitangaza kutimuliwa kwa maafisa hao.
Aidha Tume hiyo imebaini kwamba vyeti vya afisa Nelson Omwega vinaonyesha kuwa alikuwa katika darasa la nane akiwa na miaka kumi pekee.
Mwenyekiti wa NPSC Johnstone kavuludi amesema kuwa maafisa ambao wametimuliwa walijihusisha na ufisadi, utovu wa nidhamu, na ukiukaji wa haki za kibinadamu.

No comments: