Wanajeshi 14 waliookolewa kufuatia mapigano yalioshuhudiwa huko El Ade Somalia wamewasili nchini adhuhuri hii.
![]() |
| Waziri wa Ulinzi Rachael Omamo katika uwanja wa ndege wa Wilson |
Hata hivyo hamna aliyejeruhiwa kati ya 15 hao.Jeshi la Kenya linaendeleza oparesheni ya kuwasaka na kuwaokoa wanajeshi walioathirika na shambulizi la waasi wa Al shabaab katika eneo la El adde Somalia.
Mkuu wa majeshi Samson Mwathethe anasema oparesheni hiyo inaendeshwa kwa umakini ili kuzuia vifo zaidi vya wanajeshi wa Kenya.
Aidha Waziri wa ulinzi Rachael
Omamo amesema jamaa za
waathiriwa wanaendelea kufahamishwa kuhusu wapendwa waliofariki wakati wa
shambulizi hilo.
Akiongeza kuwa wameanzisha vituo maalum vya kuwahudumia jamaa
za waathiriwa katika kambi za kijeshi zilizoko Eldoret, Gil Gil na forces
memorial hapa jijini Nairobi.

No comments:
Post a Comment