Thursday, 25 February 2016

MATIANG'I AWATAKA WALIMU WAKUU KUTOA VYETI VYA WANAFUNZI

Waziri Matiang'i na wanafunzi wa shule ya upili ya wasichana ya Keveye 
Pharence Nduko

Waziri wa elimu Dkt.Fred Matiang'i amewataka walimu wakuu kutoa vyeti vya wanafunzi.

Wakurugenzi wa elimu wamepewa muda hadi mwishoni mwa mwezi kuwasilisha orodha ya shule ambazo zinashikilia hati za kukamilisha shule za wanafunzi. 
Aidha, Matiangi amewasuta wakuu wa shule ambao bado wanashikilia hati hizo kwa dai la masalio ya karo. Anasema hatua hiyo imewanyima wengi wa vijana kuendelea na masomo. Ametoa onyo kali dhidi ya wakuu watakaoendelea na tabia hiyo.

No comments: