![]() |
| Mgombea wa urais Kizza Besigye |
Gari lake lilikuwa likipitia barabara ya Jinja, mjini Kampala, msafara wake ukisindikizwa na mamia ya wafuasi, pale polisi walipotumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi hao na wakamkamata mwanasiasa huyo.
Alizuiliwa kwa muda katika kituo cha polisi lakini akaachiliwa huru bila kufunguliwa mashtaka.
Polisi wanasema alikamatwa kwa sababu ya kutatiza uchukuzi mjini.
Besigye alipangiwa kufanya mikutano ya kampeni katika mji mkuu wa Kampala.

No comments:
Post a Comment