Monday, 14 March 2016

JOHO AMWANDIKIA NKAISSERY KUTAKA RUFAA ZAIDI DHIDI YA AGIZO LA KUREGESHA SILAHA

Gavana wa Mombasa Hassan Joho na Kinara wa Cord Raila Odinga
Ben Kirui

Gavana wa kaunti ya Mombasa Ali Hassan Joho sasa amemwandikia waziri wa usalama wa ndani Joseph Nkaissery akitaka rufaa dhidi ya agizo la kuregesha bunduki alizonazo.
Kupitia wakili wake Ahmed Nassir Abdullahi, Joho amemshutumu msimamizi wa utoaji wa leseni za bunduki Samuel Kimaru akisema maagizo hayo yalitolewa kwa misingi ya kisiasa.
Joho pia anadai Kimaru alitoa agizo hilo kufuatia uchaguzi mdogo wa Malindi ambapo ODM waliwashinda Jubilee na kuitaja hatua hiyo kama kinyume cha sheria.
Wakati huo huo Kamanda mkuu wa polisi kanda ya Pwani Francis Wanjohi amekanusha uvumi unaoenea kwamba waliokuwa walinzi wa gavana wa Joho wamekamatwa na kuzuiliwa katika kituo kimoja cha polisi mjini Mombasa.


No comments: