Thursday, 3 March 2016

MAAFISA WASIMAMISHWA KAZI



By  Lena Juliet

Wizara ya masuala ya ndani imewasimamisha kazi kwa muda takriban maafisa mia moja kwa kushindwa kukabili matumizi na biashara ya pombe haramu maeneo tofauti ya nchi.
Akiongea huko kiambu katibu katika wizara hiyo Karanja Kibicho amesema kuwa manaibu wa chifu  na machifu wataachishwa kazi iwapo maeneo yao yataendelea kuendesha biashara hiyo.
Anasema maafisa hao wamekuwa wakishirikiana na watengenezaji na wauzaji wa pombe hiyo. Amekosoa idara ya mahakama kwa kukosa kutoa adhabu kali kwa wahusika.

No comments: