Thursday, 21 April 2016

MCHUNGAJI ASHTAKIWA KWA KUMNAJISI MPWA WAKE EMBU

Ben Kirui

Mchungaji wa kanisa la ACK Mbiruri kaunti ya Embu amefikishwa mahakamani hii leo kujibu mashtaka ya kumnajisi mpwa wake mwenye umri wa miaka saba.

Mchungaji huyo Elijah Gichangi hata hivyo, amekana mashtaka hayo mbele ya hakimu mkuu wa mahakama ya Embu Robinson Oigara na akaachiliwa kwa dhamana ya shillingi 100,000.

Hiyo jana mchungaji huyo alinusurika kifo baada ya wenyeji waliokuwa na ghadhabu kuvamia hospitali ya Embu level 5 ambako alikuwa amepelekwa na maafisa wa polisi kufanyiwa uchunguzi.
  

No comments: