Thursday, 21 April 2016

PESA ZA EUROBOND ZILIPOTEA CORD WADAI


Vinara wa Cord Kalonzo Musyoka, Raila Odinga na Moses Wetangula

 Ben Kirui

Muungano wa Cord umewataka wananchi kusahau fedha zilizotokana na mkopo wa Eurobond wakidai ni rasmi kwamba fedha hizo zimepotea.

Wakihutubia wanahabari hapa jijini Nairobi vinara wa muungano huo Raila Odinga, Kalonzo Musyoka na Moses Wetangula wamewataka wananchi kutotarajia kupata fedha hizo ambazo wanadai zimepotea.

Vinara hao wamefikia hatima hiyo baada ya gavana wa Benki Kuu Dkt Patrick Njoroge kukatalia mbali ombi la Raila Odinga kukutana naye kujadili matumizi ya fedha hizo.


Haya yanajiri muda mchache baada ya kinara wa Cord Raila Odinga kutishia kuchukua hatua za kisheria kumshurutisha gavana wa benki kuu kutoa maelezo kuhusiana na sakata ya Eurobond.

Raila anasema Cord pia itamchukulia hatua mwenyekiti wa benki kuu Mohamed Nyaoga kwa kumwagiza gavana kutotoa maelezo kinyume na katiba.

No comments: