![]() |
| Waziri mkuu wa Namibia Saara Amadhila |
Ben Kirui
Waziri
mkuu wa Namibia Saara Amadhila anatarajiwa kuhudhuria Kongamano la tatu la kila
mwaka la ugatuzi litakaofanyika katika kaunti ya Meru wiki ijayo.
Naibu mwenyekiti wa baraza la magavana Salim Mvurya
amesema magavana pamoja na viongozi wengine wanaalikwa.
Waziri wa ugatuzi na mipango Mwangi Kiunjuri naye amependekeza
kuwepo kwa ushirikiano kwa magavana na taasisi nyingine za serikali ili kuhakikisha
mfumo wa ugatuzi unafaulu nchini.
Rais Uhuru Kenyatta ambaye ni mgeni rasmi, naibu
wake William Ruto ni miongoni mwa wageni elfu sita kutoka kila pembe ya nchi
watakaohudhuria hafla hiyo.

No comments:
Post a Comment