Saturday, 28 May 2016

GRANIT XHAKA AJIPATA MATATANI.




Sajili mpya wa Arsenal Granit Xhaka.
Mwangi K. Githinji.


Mashabiki wameendelea kuiponza klabu ya Arsenal pamoja na sajili wake mpya Granit Xhaka.

Hii ni baada ya staa huyo kuibua madai kwamba yeye ni kiongozi, akirejelea tukio la awali ambapo mamake alikuwa akimwachia funguo za nyumba alipokuwa mchanga, licha ya kuwa na ndugu aliyemzidi umri.

Wengi kwenye mitandao ya kijamii wamemkemea sana huku baadhi yao wakimtania na kumuambia kwamba asidhani kuwa yeye ni kiongozi katika soka kwa sababu tu alipewa majukumu ya kuweka funguo katika zama hizo za utotoni.

Licha ya hayo ni wazi kuwa Xhaka aliyehama kutoka Borussia Monchengladbach ya ujerumani ni kiungo mzuri na ambaye atakiimarisha kikosi cha wanabunduki hao.


No comments: