Saturday, 28 May 2016

KIPA OTIENO KUJIUNGA NA 'INGWEE'


Kipa wa Posta Rangers Ian Otieno.
Mwangi K. Githinji.
AFC Leopards wanatarajiwa kutangaza ujio wa kipa mpya Ian Otieno kutoka Posta Rangers.
Chipukizi huyo anaripotiwa kutofautiana na kocha wake Zedekiah  Otieno hali maarufu 'Zico' na anaelezewa kuwa tayari AFC na Posta wamekubaliana kuhusu uhamisho wake.
Usajili wake ni habari nzuri kwa Ingwee ambao wamempoteza kipa wao Lucas Indeche ambaye atafanyiwa upasuaji wa bega lake huku pia wakimuangazia kipa Gabriel Andika.


No comments: