Saturday, 28 May 2016

MBWA WA ISCO ANAITWA MESSI.

Isco na mbwa wake anayeitwa Lionel Messi.


Mwangi K. Githinji.

Staa wa Real Madrid Isco amefichua kuwa mbwa wa familia yake anaitwa Lionel Messi ,sawia na nyota huyo wa Barcelona.

Isco anayetoka nchini Uhispania  anadai kuwa Messi hakumchochea kumpa jina hilo, japo alikubali kwamba yeye ni shabiki mkubwa wa Messi.

Kulingana na mchezaji huyo wazo la kumpa jina hilo lilitoka kwa babake na kakake ila sio kwake.

Alisema mbya huyo yuko na wazazi wake kwa sasa, huku akieleza kuwa ameacha kutembea naye 
kwenye mitaa ya Madrid kwa sababu ni kinaya kwake kumuita jina hilo mbele ya umma hasa ikikumbukwa kwamba  wengi wanaoishi huko ni mashabiki wa Real Madrid.


Hivyo basi anaogopa kuwa huenda  tendo hilo  likaibua mgogoro baina yake na wafuasi hao.

No comments: