Sunday, 22 May 2016

SIJAWAI KUONDOKA NA SITAONDOKA JUBILEE, AKIRI ISAAC RUTO


Gavana wa Bomet Isaac Ruto

Ben Kirui

Gavana wa Bomet Isaac Ruto, amepuuzilia mbali wakosoaji wake na kusisitiza kwamba angali ndani ya Jubilee na kusema hajawahi kuondoka na hataondoka kwenye muungano huo.

Akizungumza na wanahabari nyumbani kwake, Ruto amesema tofauti zinazokisiwa kuwepo kati yake na Naibu Rais William Ruto ni sintofahamu iliyoundwa na wabunge wa eneo hilo ambao wameamua kuendeleza ajenda zao bila kumshirikisha.

Gavana Ruto amekuwa akionekana kukosoa serikali ya Jubilee huku kwa mara nyingi akitofautiana na Naibu Rais William Ruto hadharani.
 

No comments: