![]() |
| Cord waendeleza shinikizo za kutaka makamishna wa IEBC kung'atuka |
Ben Kirui
Wafuasi wa mrengo wa upinzani Cord
wamekaidi amri ya serikali na kuandamana katika afisa za tume ya uchaguzi na
maeneo mipaka nchini IEBC kushinikiza maafisa wa tume hiyo kujiuzulu.
Ilibidi maafisa
wa polisi hapa jijini Nairobi kutumia vitoa machozi kuwatawanya waandamanaji wa
muungano wa Cord waliokuwa wameandamana hadi afisi za tume hiyo
Kiongozi wa
Cord Raila Odinga anashikilia kuwa makamishna wa IEBC hawawezi kusimamia
uchaguzi huru na wa haki mwaka ujao.
Hii ni mara
ya pili kwa muungano huo kufanya maandamano hadi afizi za IEBC huku muungano
huo ukishikilia kwamba wataendelea na shinikizo za kutaka makamishna wa IEBC
kung'atuka.

No comments:
Post a Comment