![]() |
| Wachezaji wa Wazito Fc wakisherehekea bao. |
Na Mwangi K. Githinji.
Mechi za ligi ya daraja la kwanza ziliendelea hii leo ambapo Wazito FC waliwacharaza Shabana ambao wamo kwenye nafasi ya mwisho mabao
3-0 katika mechi iliyochezewa ugani wa Awendo Green Stadium.
Kabla
ya mchezo huo Wazito walikuwa wamepoteza mechi zao tatu zilizopita huku nao
Shabana wakiwa bado hawajashinda mechi yeyote hadi sasa.
Zoo Kericho nao waliwashinda KCB mabao 4-1 huko Kericho Green
Stadium.
Katika maeneo ya Naivasha ,wenyeji Oserian walilazimishwa kutoka sare ya
kutofungana kwenye mchezo uliokuwa wa kusisimua japo timu zote mbili
zilishindwa kuzitumia nafasi zao vizuri.

No comments:
Post a Comment