Wednesday, 15 June 2016

CORD YAFUTILIA MBALI MAANDAMANO YA ALHAMISI


Viongozi wa Cord James Orengo na Johnstone Muthama wakihutubia wanahabari awali


 Ben Kirui

Muungano wa Cord umefutilia mbali maandamano yaliyokuwa yameratibiwa kufanyika katikati ya jiji hii leo.


Viongozi wa cord wamesema wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya wenzao wa jubilee kuonyesha nia njema katika mchakato wa mazungumzo kutafuta suluhu wa utata unaokabili tume ya uchaguzi na maeneo mipaka nchini IEBC.

Hata hivyo Wanakamati simamizi katika muungano wa Cord James Orengo na Esely Simiyu wanaonya kwamba maandamano hayo yatarejelewa jumatatu na alhamisi ijayo endapo mazungumzo hayo hayatazaa matunda.
 

No comments: