Thursday, 23 June 2016

FYATENI ULIMI-MKE WA VARDY.


Mke wa Vardy Rebekah.
Na Mwangi K. Githinji.

Baada ya mchezaji wa Leicester City Jamie Vardy kusaini mkataba mpya na klabu hicho sasa mke wake amewaponza baadhi ya mashabiki wa Leicester na Arsenal ambao walimkemea wakati mume wake alikuwa anahusishwa na kwenda Emirates.

Rebeka amewasuta mashabiki hao ambao walikuwa wameamini kwamba Vardy alikuwa ameghuria Arsenal na hasa waliomtuhumu kuwa ndiye alikuwa amemshawishi aondoke  huku akiwaonya kuwa wanafaa kuomba msamaha.

Awali ilikuwa imeripotiwa kuwa Vardy alikuwa amekubali kujiunga na Arsenal kwa ada ya yuro milioni 20.


Lakini amewashukuru wote ambao waliendelea kumuunga mkono.

No comments: