Tottenham wanakaribia kumaliza
uhamisho wa mchezaji wa Southampton na timu ya taifa ya Harambee Stars Victor Mugubi Wanyama.
Inaaminika kuwa Southampton wakamruhusu
aondoke ila tu iwapo watalipwa kima cha yuro milioni12 ambacho walilipa wakati
ambapo walimsajili kutoka klabu cha Celtic.
Tottenham walijaribu kumsajili msimu jana mnamo mwezi wa
agosti lakini timu yake ikadinda kumuuza.
Iwapo atasajiliwa basi ataungana na
aliyekuwa meneja wake wa zamani Mauriccio Pochettino Ronald Koeman huku wakiwa
na imani kuwa ujio wake utakipiga jeki kikosi chao.

1 comment:
Naunga mkono uhamisho huo.
Post a Comment