Sunday, 5 June 2016

NEYMAR BADO HAJATOSHA MBOGA- PELE.

Mchezaji wa Barcelona Neymar Da Silva.
Mwangi K. Githinji.
Kigogo wa Brazil Pele ameibua madai kuwa mchezaji Neymar da Silva bado hajafikia viwango vya mastaa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.
Nyota huyo wa Barcelona alikuwa watatu nyuma ya mastaa hao wawili katika tuzo za mwaka jana za Ballon d'Or na wengi wameeleza kuwa huenda akaishia kuwa mchezaji bora zaidi duniani.
Japo Pele amekuwa akimtaja Neymer kama mchezaji mzuri amekubali kuwa itamchukua muda kufikia viwango vya Messi na Ronaldo akiongeza kuwa Messi ni ndiye mchezaji bora zaidi kumshinda Ronaldo.
Neymar kwa sasa hajajumuishwa kwenye kikosi cha Brazil kinachoshiriki mashindano ya Copa Amerika lakini anatarajiwa kuwachezea kwenye michezo ya Olimpiki itakayofanyika Rio de jeneiro

.

No comments: